Thursday, December 27, 2012

MAREKANI INA IDADI KUBWA YA WATOTO WAISHIO BILA BABA


Imebainika kuwa takribani watoto milioni 15 nchini Marekani wanaishi bila baba zao hii ikiwa ni mtoto moja katika kila watoto watatu nchini humo.
Kwa mujibu wa  ripoti ya Idara ya Takwimu Marekani, tatizo la kutoweka baba katika familia linaonekana zaidi katika familia za Wamarekani wenye asili ya Afrika ambapo idadi hiyo ni karibu watoto milioni tano. Wataalamu wa masuala ya jamii wanasema tatizo hilo limepelekea kuongezeka umasikini, uhalifu na utumizi wa madawa ya kulevya Marekani.
Vincent DiCaro Mkuu wa Jumuiya ya Kitaifa ya Kinababa anasema matatizo mengi ya Marekani yanaweza kutatuliwa iwapo wazazi wote wawili wataishi pamoja. Kwa mujibu wa uchunguzi wanandoa wanaoishi pamoja Marekani huwa na pato la takribani dola thamanini elfu kwa mwaka huku akina mama waishio bila waume zao wakiwa na pato la takribani dola 24 elfu kwa mwaka.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO