Thursday, December 27, 2012

WAANDAMANAJI WAFUNGA KITUO CHA MAFUTA


Waandamanaji nchini Libya wamesababisha kufunguwa kituo kikubwa cha kuhifadhi mafuta ghafi ya petroli mashariki mwa nchi hiyo. Naibu Waziri wa Mafuta Libya Omar Shakmak amesema wasimamizi wa Bandari na Kituo cha Mafuta cha Zueitina wameamua  kufunga kituo hicho kwa kuhofia hujuma ya waandamanaji. 'Waandamanaji wanataka serikali iwape nafasi za kazi na wanaamini kuwa wanaweza kuishinikiza serikali kwa kusimamisha shughuli za mashirika  ya uchimbaji mafuta ya petroli', amesema naibu waziri wa mafuta Libya Bandari ya Zueitina husafirisha nje karibu mapipa 60,000 ya mafuta ghafi kila mwaka.
Kwa ujumla Libya husafirisha nje mapipa milioni moja laki sita ya mafuta ghafi kila siku. Tatizo na ukosefu wa ajira ni kati ya changamoto kubwa za viongozi wa Libya ambao wamechukua madaraka nchini humo baada ya kutimuliwa madarakani Muammar Gaddafi aliyeuawa katika mapinduzi ya wananchi yaliyojiri nchini humo mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO