Sunday, December 30, 2012

MAREKANI SUALA LA FEDHA BADO TATA


Duru za habari kutoka Marekani zinaarifu kuwa, viongozi wa kisiasa wa vyama vya Republican na Democrats wameendelea kulumbana kutokana na kushadidi kwa hali mbaya ya uchumi wa nchi hiyo. Sintofahamu hiyo imetokea kuhusiana na juu ya namna gani ya kutatua matatizo hayo ya kiuchumi ili kuweza kuwapunguzia wananchi wa nchi hiyo mzigo wa mgogoro wa kiuchumi. Mkuu wa taasisi ya Centre for Corporate Policy iliyopo mjini Washington Bwana Charlie Cray amesema kuwa, jamii ya watu wa tabaka la kati nchini Marekani, ndio wahanga wa malumbano ya kisiasa nchini humo. Ameongeza  kuwa, hali hiyo imezidisha ongezeko la ukosefu wa ajira na mgogoro wa kiuchumi. Mtaalamu huyo wa masuala ya kiuchumi pia amesisitiza kuwa, hali mbaya zaidi inawakabili Wamarekani wenye asili ya Kiafrika na kwamba kiwango cha ukosefu wa ajira katika tabaka hilo kimefikia asilimia 12.4, ambapo wengi wao ni vijana walio na umri wa kati ya miaka 18 hadi 29.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO