Sunday, December 30, 2012

WAPALESTINA WASHAMBULIWA NA HOMA YA H1N1


Kwa akali Wapalestina 9 wamefariki dunia kutokana na kukumbwa na aina ya kutisha ya homa ya H1N1 katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan huko katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Hapo jana viongozi wa Palestina walitangaza kuwa, Wapalestina hao walifariki dunia katika kipindi cha wiki mbili zilizopita baada ya kukumbwa na homa ya H1N1. Viongozi hao wamesisitiza kuwa, hadi sasa Wapalestina wengine wapatao 189 wameathirika na homa hiyo katika eneo hilo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Viongozi wa Palestina pia wametangaza kuwa, tayari Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO limekubali kutuma chanjo kwa ajili ya kukabiliana na homa ya H1N1.

Yaa rabbi wape shifaa yako ndugu zetu hawa na uwape nguvu ya kuitetea nchi yao na uislam kwa ujumla AAMin

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO