Saturday, December 29, 2012

SAIF ISLAM KUFIKISHWA MAHAKAMANI MWEZI UJAO


Mwana wa kiume wa dikteta wa zamani wa Libya Saiful Islam Gaddafi na mkuu wa zamani wa vyombo vya ujasusi vya nchi hiyo Abdullah Sanoussi watafikishwa mahakamani mwezi ujao. Msemaji wa Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Libya Taha Bar'a amesema kuwa kesi ya Seiful Islam na Sanoussi itafanyika mwezi ujao mjini Tripoli licha ya wito wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) inayotaka ikabidhiwe mwana huyo wa Gaddafi.
Msemaji wa mahakama ya ICC Fadi al Abdullah amesema mahakama hiyo ya kimataifa italichukua faili la kesi ya Saiful Islam Gaddafi iwapo mahakama za Libya hazitasimamia kesi yake kwa uadilifu. Ameongeza kuwa viongozi wa Libya wameahidi kwamba wataheshimu sheria za kimataifa katika uendeshaji wa kesi hiyo. Saiful Islamu Gaddafi anakabiliwa na tuhuma za kutenda jinai dhidi ya binadamu na jinai za kivita.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO