Friday, December 28, 2012

MAREKANI KUANZA VIKAO MASUALA YA KIFEDHA


Rais wa Marekani Barack Obama leo ataongoza mkutano wa viongozi wa bunge ikiwa ni pamoja na mahasimu wake wakuu wa chama cha Republican katika jitihada za mwisho za kuizuia Marekani kuelekea katika kile kinachofahamika kama mkwamo wa kiuchumi.
Afisa wa Ikulu ya White House amesema Obama atakutana na mahasimu wake wa Republican Spika wa Baraza la wawakilishi John Boehner na Kiongozi wa upande wa viti vichache katika Seneti Mitch McConnell na washirika wake wa Democratic Kiongozi wa upande wa viti vingi katika Seneti Harry Reid, na Kiongozi wa upande wa viti vichache katika Baraza la Wawakilishi Nancy Pelosi. Mkutano huo unakuja wakati kukiwa na ongezeko la mvutano wa kisiasa na kuongezeka wasiwasi nchini Marekani kuhusu kama muafaka dhabiti utaweza kupatikana kabla ya kumalizika mwaka huu ikiwa ndio muda wa mwisho. Siku ya Jumatano Obama alizungumza na viongozi hao wanne McConnell, Reid, Boehner na Pelosi akitaraji kusonga mbele katika mpango huo lakini wabunge na wasaidizi wao wamesisitiza kwamba hakuna hatua zozote zilizopigwa wakati wa msimu huu wa likizo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO