Friday, December 28, 2012

WAASI WA MALI WATISHIA KUWAUWA VIONGOZI WA DINI

Viongozi wengi wa dini ya Kiislamu nchini Mali, wamepatwa na wasi wasi kufuatia vitisho vilivyotolewa na makundi ya waasi wa kaskazini mwa nchi hiyo dhidi yao. Duru za habari zinaarifu kuwa, viongozi wengi wa Kiislamu akiwemo sheikh Chérif Ousmane Madani Haïdara mmoja wa masheikh mashuhuri wa nchini Mali, wanakhofia maisha yao kufuatia vitisho hivyo. Leo sheikh Ousmane amenukuliwa akisema kuwa, siku kadhaa zilizopita alipata vitisho vya moja kwa moja au visivyo moja kwa moja kupitia jamaa zake wa karibu, akitishiwa maisha yake kutoka kwa makundi ya kigaidi nchini humo. Kiongozi huyo wa kidini ambaye anaongoza taasisi moja ya kidini yenye wafuasi wengi wa Kiislamu amelieleza shirika la habari la Kifaransa kuwa, Waislamu wa Mali wanapinga vitendo na mienendo ya makundi hayo ya kigaidi na kwamba, vitendo vya kigaidi vinapingwa na dini tukufu ya Kiislamu. Baada ya mapinduzi ya kijeshi yaliyojiri mnamo tarehe 22 Machi nchini Mali, makundi ya Tuareg na Ansarud-Din, yalilishikilia eneo la kaskazini mwa nchi hiyo na kuanzisha oparesheni za kuharibu turathi za Kiislamu nchini humo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO