Friday, December 28, 2012

ASKOFU MKUU WA LEBANON AUKUBALI MPANGO WA IRAN JUU YA SYRIA

Askofu Mkuu wa Lebanon John Maron amekaribisha mpango wenye vipengele sita ulioandaliwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kwa ajili ya kumaliza mgogoro wa kisiasa nchini Syria. Askofu Maron aliyasema hayo leo alipokutana na Balozi wa Iran nchini Lebanon Ghazanfar Rokn Abadi na kusema kuwa, mpango huo wenye vipengee sita kwa ajili ya kumaliza mgogoro wa Syria, ni hatua muhimu kwa ajili ya nchi hiyo na eneo zima kwa ujumla. Kwa upande wake Balozi Ghazanfar, ametoa pongezi kwa mnasaba wa sherehe za kuadhimisha kuzaliwa Nabii Issa (as) na kusema kuwa, Syria itakuwa mhimili mkubwa wa kuimarisha usalama na uthabiti wa eneo ikiwemo Lebanon. Mpango huo wa amani ulioandaliwa na Iran, ulianza kusambazwa hivi karibuni na Wizara ya Mambo ya Nje kwa pande mbalimbali husika nchini Syria na eneo zima la Mashariki ya Kati kwa ujumla.  

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO