Sunday, December 30, 2012

WAPALESTINA YAIKOSOA MAREKANI

Mamlaka ya Ndani ya Palestina imeikosoa Marekani kwa kuwashinikiza Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Kiarabu wasimamishe safari yao ya kutembelea Ukingo wa Magharibi wa Mato Jordan. Ukosoaji huo umetolewa baada ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi 4 za Kiarabu kukataa kuandamana na Waziri Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu Nabil al Arabi katika safari yake ya kwanza ya kutembelea Ramallah. Wasel Abu Yussuf afisa wa ngazi za juu wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) amesema, Wamarekani wamewazuia mawaziri hao wa Kiarabu kutembelea Ramallah na kwamba Marekani na Israel zilizitaka nchi za Kiarabu kuwawekea vikwazo vya kifedha Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan baada ya kupigwa kura ya kutambuliwa Palestina kama nchi isiyokuwa mwanachama katika Umoja wa Mataifa mwezi uliopita. Al Arabii aliyetembelea Ramallah ili kujadili matatizo ya kifedha yanayoikabili Palestina, alirejea nyumbani haraka baada ya kuahidi kuisaidia Mamlaka ya Ndani ya Palestina.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO