Thursday, January 31, 2013

DAVID CAMERON ZIARANI LIBYA

Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, amefanya ziara ya kushitukiza nchini  Libya hivi leo, ziara  inayokuja  siku chache  baada  ya  Uingereza  kutoa  tahadhari  kuhusu vitisho  vinavyoukabili  ubalozi  wake  mjini  Tripoli. Cameron amewasili  mchana  wa  leo huku  kukiwa  na ulinzi  mkali. Akiongozana  na   waziri  wa  mambo  ya ndani  wa  Libya  Ashur Shwayel, Cameron  alikwenda moja  kwa  moja  katika  chuo  cha  mafunzo  ya  polisi kusini  mwa  mji  mkuu  Tripoli, ambako  alihudhuria sherehe  ya kupandishwa  vyeo kwa maafisa wa polisi. Maafisa  wa  serikali  ya  Libya wameliambia  shirika  la habari  la  AFP  kuwa  ushirikiano  katika  nyanja  ya usalama  utakuwa  katika  ajenda  ya  juu  katika mazungumzo  baina  ya  Cameron  na  maafisa  wa  Libya. Ofisi  ya  waziri  mkuu  mjini  London  imesema  kuwa Cameron  amekwenda  nchini  Libya  kujadiliana  juu  ya namna Uingereza  inavyoweza  kuendelea kusaidia  ujenzi wa  Libya imara, yenye  maendeleo  na  demokrasia.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO