Saturday, January 26, 2013

MAANDAMANO YA KUPINGA UTOAJI MIMBA YAFANYIKA MAREKANI


Maelfu ya wanaharakati wa haki za kuishi nchini Marekani jana Ijumaa wamekusanyika kwenye Mahakama Kuu nchini humo kupinga uamuzi wa kihistoria wa miaka 40 iliyopita wiki hii ambao umehalalisha utoaji mimba. Waandaaji wa matembezi ya mwaka kuhamasisha haki ya kuishi,huko Washington kwenye jengo la taifa la manunuzi,walitarajia umati mkubwa kupita ule uliojitokeza mwaka jana wa watu wapatao laki nne pamoja na uwepo wa baridi kali kwa sasa.
Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Benedicto wa 16 ameunga mkono maandamano hayo kwa kutuma ujumbe mfupi kupitia anwani yake ya mtandao wa twiter akiwatakia kila la heri wanaharakati hao na kusema kuwa anawaombea viongozi wa kisiasa ili walinde maisha ya watoto ambao bado hawajazaliwa na kuhamasisha utamaduni wa maisha.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO