Saturday, January 26, 2013

VIKOSI VYA UFARANSA VYASONGA MBELE MALI

Vikosi vya Ufaransa na Mali vimesonga mbele kuelekea ngome muhimu ya waasi wenye itikadi kali za Kiislamu ya Gao, baada ya kuudhibiti tena mji wa kaskazini wa Hombori. Duru za vikosi vya usalama zimeeleza kuwa wanajeshi hao wataelekea Gao, moja ya miji mikubwa mitatu iliyopo eneo la kaskazini, ambako waasi wenye mafungamano na Al-Qaeda wameanzisha sheria ya Kiislamu ya Sharia kwa miezi kumi. Kwa mujibu wa duru hizo, katika eneo la magharibi mwa Mali, vikosi vinavyoongozwa na Ufaransa vinaelekea kwenye mji wa Lere kwa lengo la kuudhibiti mji wa Timbuktu uliopo kaskazini. Wakati huo huo, wakuu wa majeshi wa nchi za Afrika Magharibi wanakutana leo mjini Abidjan, Cote d'Ivoire katika kikao cha dharura kujadili operesheni za kijeshi nchini Mali zenye lengo la kuwaondoa waasi hao, ambapo watatathmini mchakato unaoendelea wa kupeleka vikosi vya kimataifa nchini Mali vinavyoongozwa na Afrika vya AFISMA. Aidha, viongozi wa Umoja wa Afrika wanatarajia kukutana Jumanne ijayo katika mkutano wa wafadhili ili kujadiliana kuhusu suala la kuongeza fedha katika operesheni za Mali. Mkutano huo utawajumuisha wawakilishi kutoka Umoja wa Ulaya na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO