Saturday, January 26, 2013

MAREKANI HAWAJAAFIKIANA KUHUSU SILAHA


Duru za habari kutoka Marekani zinaarifu kuwa, wapingaji na waungaji mkono wa uuzwaji silaha za moto nchini humo wameshindwa kuafikiana kuhusiana na kadhia ya kupiga marufuku uuzaji wa silaha hizo nchini humo. Duru za habari kutoka Congress ya Marekani zinasema kuwa bunge hilo Marekani linajadili muswada wa marufuku ya uuzwaji silaha unaofahamika kwa jina la Fainstein, ambao kama utapitishwa utapiga marufuku uuzwaji wa aina 160 ya silaha kwa raia nchini humo. Mkuu wa Kamisheni ya Wananchi mjini New York anayehusika na mpango wa kukabiliana na vitendo vya jinai Richard Aybom amesema kuwa, muswada wa huo wa Fainstein ni moja ya juhudi za Rais Barack Obama wa Marekani za kupunguza vitendo vya mauaji vilivyoshika kasi zaidi katika siku za hivi karibuni nchini humo. Wakati huo huo Eric Pratt Kiongozi Mkuu wa Mahusiano ya Umma katika Taasisi inayohusika na watu wanaomiliki silaha nchini Marekani amesema kuwa, kwa uzoefu wake muswada huo hauwezi kumaliza vitendo vya jinai na mauaji vinavyotokana na silaha zinazomilikiwa na raia nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO