Saturday, January 26, 2013

HATUA YA KOREA KASKAZINI KUJARIBU SILAHA ZAKE YATIA KIWEWE NCHI ZA MAGHARIBI

Hatua ya jana ya Korea Kaskazini ya kutangaza nia yake ya kufanyia majaribio ya nyuklia kama hatua ya kukabiliana na vitisho vya Marekani, imeutia kiwewe na woga mkubwa Umoja wa Ulaya na Marekani. Bi. Catherine Ashton, Mkuu wa Siasa za Mambo ya Nje wa Umoja wa Ulaya, ameitaka Korea Kaskazini kuachana na nia yake hiyo na kufuata mkondo wa kisiasa na kufanya mazungumzo na jamii za kimataifa. Jana ikulu ya Marekani pia ilitangaza kuwa, mpango wa Korea Kaskazini wa kufanya majaribio ya nyuklia, unatia wasiwasi mkubwa na kwamba, hatua hiyo itapelekea kutengwa kimataifa nchi hiyo. Msemaji wa Ikulu ya Marekani Jay Carney aliwaambia waandishi wa habari kuwa, hatua ya Pyongyang ya kutangaza nia yake kufanya majaribio ya nyuklia, inapingana na azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Kwa upande wake Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Hung Lee, amezitaka nchi husika kukaa kwenye meza ya mazungumzo na Korea Kaskazini na kusisitiza kuwa, hiyo ndio njia pekee ya kumaliza mzozo uliopo. Hii ni katika hali ambayo, hivi karibuni Washington ilifanya jaribio la silaha za maangamizi ya umati chini ya ardhi huku jamii ya kimataifa ikiendelea kuwa bubu mbele ya hatua kama hizo za Marekani.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO