Wednesday, January 09, 2013

UPINZANI WAITAKA MAHAKAMA KUTOA TAMKO JUU YA CHAVEZ


Upinzani  nchini  Venezuela  umesema  kuwa  unakwenda mahakamani  kuitaka  mahakama  kuu  kuamua  iwapo katiba  ya  nchi  hiyo  inaruhusu  kucheleweshwa  kwa sherehe  za  kuapishwa  rais  Hugo  Chavez  ambaye anaugua  ugonjwa  wa  saratani. Tangazo  hilo  la  kiongozi wa  upinzani  Ramon Guillermo Aveledo   limekuja  baada ya  bunge  la  nchi  hiyo  kupiga  kura  kuahirisha  sherehe za  kuapishwa  kwa  Chavez, ambako  kumepangwa kufanyika  kesho  Alhamis. Makamu  wa  rais  Nicolas Maduro amesema  kuwa  ataiongoza  nchi  hiyo  hadi  pale rais Chavez  atakaporejea.
Aveledo  hakusema  ni  lini  ama  ni  vipi  upinzani unaazimia kuyafikisha  madai  yake  hayo  mahakamani. Rais  wa  mahakama  kuu  Luisa Estella Morales anatarajiwa  kuwa  na  mkutano  na  vyombo  vya  habari leo na  anaweza  kuzungumzia  jukumu  la  mahakama katika  mzozo  huo.
             

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO