Sunday, January 27, 2013

VITONGOJI VINAZUIA KUUNDWA TAIFA LA PALESTINA

Balozi wa Jordan nchini Marekani amesema kuwa, kuendelea ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi huko katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, kunazuia kuundwa kwa taifa huru la Palestina. Mwana mfalme Zaid bin Ra'ad aliyasema hayo jana katika mahojiano aliyofanyiwa na televisheni ya Bloomberg na kusisitiza kuwa, kuendelea kwa ujenzi huo wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni, kunalifanya suala la kuundwa taifa la Palestina kuwa lisilowezekana. Amesema, kuongezeka nafasi ya haki ya taifa la Palestina katika Umoja wa Mataifa, kunaonyesha mustakbali mzuri kwa Wapalestina na kwamba, kwa hatua hiyo Wapalestina wataweza kuiweka Israel katika mashinikizo. Aidha kiongozi huyo wa Jordan amesema kuwa, Wapalestina sasa wanaweza kuuburuza utawala bandia wa Kizayuni katikaMahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC. Hivi karibuni Mjumbe mwandamizi wa Harakati ya Palestina Fat'h anayeshughulikia masuala ya utungaji sheria alikosoa vikali hatua ya kuendelea ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni na kuitaka Kamisheni ya siasa za Mambo ya Nje ya Umoja wa Ulaya kuitisha kikao mwezi Machi na kujadili kwa kina suala hilo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO