Sunday, January 27, 2013

SHIRIKA LA MAFUTA LA UFARANSA KUNUNUA MAFUTA TOKA IRAN

Shirika la mafuta la Ufaransa na Korea Kusini lijulikanalo lama Samsung Total limeanza tena kununua mafuta ghafi ya petroli ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, baada ya kupata hasara kubwa iliyotokana na vikwazo vya upande mmoja vya nchi za Magharibi hasa Marekani dhidi ya Iran. Ripoti hiyo imeongeza kwa mashirika hayo yalipata hasara baada ya kuzuiwa kununua mafuta ya Iran. Hasara hiyo inayokadiriwa kufikia kiasi cha zaidi ya dola milioni 6.5, hali iliyoyalazimu kuachana na mashinikizo ya Marekani na Magharibi na hivyo kuanza tena shughuli za ununuzi wa mafuta ya nchi hii. Hatua hiyo inahesabiwa kuwa moja ya hatua za kususia vikwazo dhidi ya mafuta ya Iran kwa wateja wa mafuta hayo, sambamba na kuendelea mbinyo wa Wamagharibi kwa wateja wa Tehran. Baada ya kusimamishwa bidhaa ya mafuta ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwenda kwa wateja wake kama vile Japan na Korea Kusini, wateja mbalimbali wa bidhaa hiyo muhimu wameanza kufuatilia njia za ununuzi wa mafuta ya Iran mbali na vikwazo hivyo vya maadui wa Tehran.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO