Wednesday, January 30, 2013

WAMAGHARIBI WAZUSHA HITILAFU BAINA YA WAISLAM


Mjumbe wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni katika Bunge la Iran amesema kuwa, nchi za Magharibi zinazusha hitilafu baina ya Waislamu kwa lengo la kuvuruga na kutokomeza umoja na mshikamano wa Waislamu.
Akielezea njama zinazofanywa na  nchi za Magharibi kwa lengo la kuzusha mifarakano kati ya Waislamu ulimwenguni, Ahmad Bakhshayesh Ardistani ameongeza kuwa, awali Marekani ilikuwa ikiyaunga mkono makundi ya kigaidi kama al Qaeda na hivi sasa inatuma majeshi yake kwenye nchi mbalimbali duniani kwa kisingizio eti cha kupambana na makundi hayo. Ardistani ameongeza kuwa, mifarakano mingi inayojitokeza katika ulimwengu wa Kiislamu, inasababishwa na umasikini wa kiutamaduni wa baadhi ya jamii ya Waislamu unaowatumbukiza Waislamu kwenye mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO