Wednesday, January 30, 2013

BOKO HARAM WATAKA USITISHAJI VITA


Mmoja kati ya makamanda wa kundi la Boko Haram nchini Nigeria ametaka kusitishwa vita na serikali ya nchi hiyo. Akizungumza kwa niaba ya kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakar Shikau, Sheikh Abu Muhammad bin Abdulaziz amesema kuwa, uamuzi huo umechukuliwa kufuatia uharibifu mkubwa na maafa wanayopata wananchi wasio na hatia. Ameongeza kuwa, uamuzi huo pia unatokana na mazungumzo yaliyofanyika hivi karibuni kati ya kundi hilo na viongozi wa jimbo la Borno ambalo ni chimbuko la kundi hilo. Kundi la Boko Haram limetoa ujumbe likiwataka wafuasi wake waweke chini silaha zao.
Kwa upande mwingine, serikali ya Nigeria imekataa kuzungumza chochote kuhusiana na taarifa hiyo iliyotolewa na kundi la Boko Haram la kusitisha mapigano. Mashirika ya Kutetea Haki za Binadamu yanasema kuwa, maelfu ya watu wameuawa na majengo kadhaa ya serikali kama vile, mashule, mahospitali na vituo vya polisi kubomolewa tokea yalipoanza mashambulizi ya kundi la Boko Haram mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO