Wednesday, January 30, 2013

WANAMGAMBO WA ALQAEDA WAUAWA YEMEN

Jeshi la Yemen limefanya mashambulizi kwenye maficho ya mtandao wa al Qaeda na kuwaua wanamgambo 16 wa kundi hilo. Jeshi la Yemen jana liliwaua wanachama 16 wa al Qaeda baada ya kushambulia maficho ya kundi hilo katika eneo la Manaseh katika mkoa wa Bayda. Katika mashambulizi hayo wanajeshi wawili wa Yemen pia waliuliwa. Jeshi la Yemen lilifanya shambulio hilo dhidi ya maficho ya wapiganaji wa al Qaeda katika mkoa wa bayda kwa lengo la kuwakomboa raia wa nchi za Ulaya waliokuwa wametekwa nyara na kundi hilo.  Jana hiyo hiyo askari polisi usalama wa Yemen wasiopungua 11 waliuawa baada ya gari lililokuwa limetegwa bomu kulipuka karibu na kituo kimoja cha kijeshi cha upekuzi  katika mji wa Rida'a umbali wa kilomita 160 kusini mwa Sana'a mji mkuu wa Yemen.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO