Wednesday, January 30, 2013

JESHI LA SEPAH LAFANYA MAZOEZI GHUBA YA UAJEMI


Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC kimeanza maneva ijulikanayo kama 'Fat'h 91' katika Ghuba ya Uajemi. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Fars, mazoezi hayo yameanza leo Jumatano na yataendelea kwa siku tatu kwa lengo la kuimarisha mipango ya kujihami na kukabiliana na vitisho kwa kutumia mbinu zisizo za kawaida.
Aidha katika luteka hiyo maafisa wenye uzoefu IRGC watatoa mafunzo kwa kizazi kipya. Kamanda wa Eneo la Tatu la Kitengo cha Wanamaji cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu Admeli Seifullah Bakhtiarivan amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina uwezo mkubwa wa kijeshi. Amesema Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu wanatumia stratijia ya kujihami ya pande zote kwa kuzingatia hali hatari zaidi inayoweza kujitokeza. Hivi karibuni pia Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran lilifanya mazoezi makubwa katika eneo pana la fukweni, baharini na angani kwenye lango la Hormuz, Bahari ya Oman, kaskazini mwa Bahari ya Hindi, Ghuba ya Aden na lango la Babul Mandab. Wakuu wa vikosi vya kijeshi vya Iran wanasisitiza mara kwa mara kuwa mazoezi ya jeshi la Iran yana ujumbe wa urafiki na udugu kwa mataifa rafiki na onyo kali kwa maadui.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO