Thursday, January 31, 2013

WAPINZANI MISRI WATAKA MAZUNGUMZO NA MURSI


Muhammad al Baradei shakhsia wa upinzani nchini Misri ametaka kufanyike mazungumzo ya haraka kati ya makundi ya kisiasa na Rais Muhammad Mursi wa nchi hiyo ili kuhitimisha mgogoro wa kisiasa nchini humo. Al Baradei amesema kuwa harakati ya upinzani ya National Salvation Front inataka kufanyike mazungumzo ya haraka na Rais, pamoja na Mawaziri wa Ulinzi na Mambo ya Ndani ili kukomesha machafuko na kuanza mazungumzo ya kitaifa.
Wito huo umetolewa siku mbili baada ya kundi hilo la upinzani kukataa mwaliko wa Rais wa Misri wa mazungumzo ya kutatua matatitizo ya kisiasa na machafuko. Machafuko yalianza tena hivi karibuni katika miji kadhaa ya Misri baada ya mahakama ya nchi hiyo kutoa hukumu ya kunyongwa watu 21 waliohusika na tukio lililopelekea kupoteza maisha watu 74 baada ya mechi ya soka mwaka jana katika mji wa Port Said.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO