Thursday, January 31, 2013

ISRAEL YASHAMBULIA KITUO CHA UTAFITI CHA SYRIA


Jeshi la Syria limetangaza kuwa watu wawili wameuawa na wengine watano kujeruhiwa baada ya ndege za kijeshi za utawala wa Kizayuni wa Israel kushambulia kituo cha utafiti wa sayansi cha Jamraya karibu na mji mkuu Damascus.
Taarifa ya jeshi la Syria imeeleza kuwa, ndege za Israel zilikiuka anga ya Syria jioni ya Jumatano na kushambulia moja kwa moja kituo cha utafiti wa sayansi ambacho kinaisaidia Damascus kuimarisha muqawamma na kujilinda. Utawala wa Kizayuni umedai kwamba ulilenga msafara uliokuwa umebeba silaha za kemikali nchini Syria. Jeshi la Syria limesema, mashambulizi hayo ni mfano mwingine wa jinai za Israel na utumiaji mabavu dhidi ya Waarabu na Waislamu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO