Thursday, January 31, 2013

WATU 80 WAFARIKI MAFURIKO MSUMBIJI


Mafuriko mapya yameripotiwa nchini Msumbuji ambapo watu saba wameuawa na hivyo kupelekea idadi ya watu waliouawa katika mafurko ya hivi karibuni nchini humo kufika 80 na wengine 250,000 kuachwa bila makao.
Ripoti zinasema kuwa mvua kali jana Jumatano zilipelekea karibu watu 17 elfu kuondoka makwao kati kati mwa jimbo la Zambezia na mji wa Nampula kaskazini mwa nchi hiyo. Imearifiwa kuwa mwanamke mmoja mjamzito amejifungua juu ya paa la nyumba. Mama huyo aliyetambulika kwa jina la Hortensia ni mkazi wa wilaya ya Chokwe nchini Msumbiji, moja ya maeneo yaliyoathirika zaidi na mafuriko hayo. Ripoti zinasema Hortensia alijifungua salama mtoto wa Kike akiwa juu ya paa. Maafisa wa hali ya hewa wameonya uwezekano wa kutokea mvua kubwa zaidi na wamewataka wakazi wa maeneo yaliyokumbwa na maafa kuchukua tahadhari.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO