Friday, January 25, 2013

WAZAYUNI WAMECHOCHEA MARUFUKU YA KANALI ZA IRAN

Wabunge kadhaa nchini Uhispania wameikosoa vikali serikali ya nchi hiyo kwa kupiga marufuku matangazo ya kanali za Televisheni za Press TV na Hispan TV kutokana na mashinikizo ya lobi za Kizayuni na Marekani. Katika barua yao, wabunge wa chama cha United Left wameitaka serikali ya Uhispania kutoa maelezo iwapo Waziri wa Mambo ya Nje wa Uhispania Jose Manuel Garcia-Margallo alijadili suala la kupiga marufuku kanali za Iran wakati alipokutana na lobi za Kizayuni Oktoba mwaka 2012. Wabunge hao wamesema mmiliki wa shirika la satalaiti ya Eutelsat ana uraia wa Israel na kwamba amekuwa akiongoza njama dhidi ya vyombo vya habari vya Iran barani Ulaya.
Televisheni ya Iran ya Hispan TV hurusha matangazo kwa lugha ya Kihispania kwa masaa 24 nayo Press TV hurusha matangazo yake kwa lugha ya Kiingereza. Hivi karibuni televisheni za kimataifa za Iran Hispan TV pamoja na Press TV zilipigwa marufuku kurusha matangazo yao kupitia satalaiti za Ulaya za Eutelsat na Hotbird. Aidha Shirika la Intelsat limepiga marufuku matangazo ya radio na televisheni kadhaa za kimataifa za Iran kufuatia mashinikizo ya Umoja wa Ulaya. Maamuzi hayo ya kupiga marufu vyombo vya habari vya Iran ni ishara ya wazi ya undumakuwili wa nchi za Magharibi zinazodai kutetea uhuru wa maoni. Nchi za Ulaya na Marekani zikishirikiana na utawala wa Kizayuni wa Israel zinajaribu kuzima sauti ya haki ya vyombo vya habari vya Iran.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO