Friday, January 25, 2013

KOREA KASKAZINI YATISHIA KUISHAMBULIA KUSINI

Korea Kaskazini imetishia kuishambulia Korea Kusini, kama utawala mjini Seoul utaunga mkono vikwazo vipya vya Umoja wa Mataifa dhidi ya nchi hiyo. Onyo hilo la Korea Kaskazini limetolewa wakati ambapo Marekani imetangaza vikwazo zaidi vya kiuchumi dhidi ya Korea Kaskazini, kufuatia hatua ya nchi hiyo kutuma roketi ya setilaiti angani mwezi uliyopita. Korea Kaskazini imemuonya jirani wa kusini kuwa vikwazo vinamanisha kutangaza vita dhidi yao. Korea Kaskazini ilitangaza wiki hii kususia mazungumzo yote yanayolenga kusitisha mpango wake wa nyuklia, na kuapa kufanya majaribio zaidi ya roketi na nyuklia, baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuituhumu kwa jaribio la kombora la masafa marefu Desemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO