Thursday, February 28, 2013

JESHI LA WANAMAJI WA IRAN KUZIMA NJAMA ZA MAADUI


Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Iran kwa kutumia uwezo wa jeshi lake la wanamaji litazima njama zote za maadui katika eneo hili. Admeli Habibullah Sayyari ameyasema hayo Jumanne  mjini Tehran katika Kongamano la Tiba na Shughuli za Uokozi Baharini na kuongeza kuwa, Jeshi la Wanamaji la Iran lina uwezo wa kutekeleza oparesheni katika maji ya kieneo na kimataifa. Admeli Sayyari ameendelea kusema kuwa, leo Jeshi la Wanamaji la Iran linatumia teknolojia ya kisasa kabisa katika shuguhuli zake. Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Iran amesema, mbali na kuwa na suhula za kisasa pia kunahitajika wataalamu wenye ujuzi wa hali ya juu na kwa bahati nzuri Iran imefanikiwa sana katika uwanja huo. Admeli Sayyari amesema msafara wa manowari za Jeshi la Wanamaji la Iran kwa mara ya kwanza umepita katika Lango Bahari la Malacca ambalo ni moja kati ya maeneo muhimu ya zaidi ya baharini duniani. Ameongeza kuwa msafara huo wa meli za kivita za Iran leo umeingia katika Bahari ya Pasifiki na katika siku chache zijazo meli hizo zitatia nanga nchini Uchina kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kirafiki kati ya Beijing na Tehran.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO