Thursday, February 28, 2013

WANAMGAMBO WAVAMIA OFISI YA WAZIRI MKUU WA LIBYA

Makumi ya wanamgambo wa Libya wanaohusika na kulinda amani katika baadhi ya mipaka ya nchi hiyo, wameshambulia ofisi ya Waziri Mkuu Ali Zeidan, wakilalamikia hali duni ya mishahara yao. Tukio hilo lilitokea jana Jumatatu wakati Waziri Mkuu akiwa hayupo ofisini. Habari zinasema kuwa, Waziri Mkuu wa Libya alikuwa amekwenda kushiriki kikao cha Baraza la Haki za Binaadamu cha Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Uswisi, ambapo watu wanaokadiriwa 30 walishambilia ofisi yake mjini Tripoli. Awali wanamgambo hao walikuwa wamekwenda ofisini hapo  kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu Ali Zeidan lakini walipopata habari kuwa hayupo walikasirika na kuanza kufanya fujo ofisini kwake. Wanamgambo hao wa vikosi vya ulinzi wa usalama katika mipaka ya Libya wako chini ya Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo.  Mipaka ya Libya inalindwa na wanamgambo, kutokana na nchi hiyo kudhoofika kijeshi na kipolisi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO