Sunday, February 24, 2013

WAPALESTINA WATAKA KUUNDWA TUME KUCHUNGUZA MAUAJI YA MWENZAO.


Mamlaka ya Ndani ya Palestina (PA) imetaka kufanyike uchunguzi wa kimataifa kuhusiana na kifo cha mateka wa Palestina katika jela ya Israel. Afisa wa mamlaka hiyo Issa Qaraqea amesema kwamba taarifa walizopata zinaonyesha kwamba Mpalestina huyo alifariki dunia wakati alipokuwa akihojiwa na kwamba suala hilo linaonyesha kwamba huenda alifariki dunia kutokana na kuteswa wakati wa kuhojiwa.
Mpalestina huyo Arafat Jaradat aliyekuwa na miaka 30 alifariki dunia katika jela ya Israel ya Magiddo na askari usalama wa jela hiyo wanadai kwamba, kifo chake kimetokana na matatizo ya kiafya aliyokuwa nayo. Kuna zaidi ya Wapalestina 4,500 wanaoshikiliwa katika jela na korokoro za kuogofya za utawala wa Kizayuni wa Israel bila kuhukumiwa huku wakikabiliwa na mateso na hali mbaya ya kibinadamu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO