Sunday, February 24, 2013

JESHI LA IRAN LAISHUSHA DRONE NYINGINE ILIYOKATIHS ANGA YAKE

Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC kwa mara nyingine limefanikiwa kuilazimisha kutua chini ndege isiyo na rubani (drone) ya nchi adui baada ya kuingia kwa siri katika anga ya Iran. Ndege hiyo ya kijasusi imenaswa  katika Mazoezi ya Kijeshi ya Mtume Mtukufu SAW 8 yaliyoanza jana Jumamosi kusini mwa nchi. Msemaji wa maneva hiyo Jenerali Hamid Sarkheili amewaambia waandishi habari kuwa,  ‘wataalamu wa kitengo cha vita vya kielektroniki katika IRGC walitambua ndege isiyokuwa na rubani iliyokuwa na lengo la kukiuka anga ya Jamhuri ya Kiislamu na hapo waliweza kuidhibiti na kuilazimisha kutua chini pasina kuwepo uharibifu.’ Ikumbukwe kuwa  Desemba mwaka 2011 vikosi vya ulinzi vya Iran vilkifanikiwa kuinasa ndege ya kisasa ya kijasusi ya Marekani aina ya RQ-170 iliyokuwa imeingia nchini. Aidha Desemba 4 mwaka 2012 Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu lilitangaza kuwa lilifanikiwa kunasa ndege ya kijasusi ya Marekani aina ya ScanEagle katika maji ya Ghuba ya Uajemi. Jenerali Sarkheili amesisitiza kuwa kwa kutumia uwezo huo wa vita vya kielektroniki Iran inaweza kuvuruga kwa urahisi mfumo wa makombora ya maadui. Amesema  Mazoezi ya Kijeshi ya Mtume Mtukufu SAW 8 yanalenga kuimarisha uwezo wa mbinu mpya za kivita. Jenerali Sarkheili amesistiza kuwa uwezo wa kijeshi wa Iran ni wa kujihami na kwamba Jamhuri ya Kiislamu haina nia ya kuvamia nchi nyingine. Mazoezi hayo yataendelea hadi Februari 25.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO