Thursday, February 28, 2013

ZIARA YA RAIS WA PAKISTAN IRAN YAKAMILIKA

Kongozi wa kiroho wa wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, amemtaka rais wa Pakistan, Asif Ali Zardari, kuendelea na mradi uliocheleweshwa wa mabomba ya gesi wa dola bilioni 7.5 licha ya upinzani kutoka kwa Marekani. 
Khamenei amesema mradi huo wa mabomba ya gesi kati ya Iran na Pakistan ni mfano mzuri wa ushirikiano baina ya nchi hizo mbili, licha ya hofu zilizopo. Zardari pia alikutana na rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad, ambaye alinukuliwa akisema kwamba wataendelea kuimarisha uhusiano baina yao. Mradi huo wa gesi, umekumbwa na changamoto za mara kwa mara, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa ufadhili kwa upande wa Pakistan, na upinzani mkali kutoka kwa Marekani, ambayo imeiwekea Iran vikwazo kutokana na shughuli zake za urutubishaji wa madini ya Uranium.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO