Thursday, February 28, 2013

UN KUIONDOLEA VIKWAZO VYA SILAHA SOMALI

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linajitayarisha kuiondolea Somalia vikwazo vya silaha ambavyo vimekuwa vikitekelezwa kwa miongo miwili sasa. Duru za kidiplomasia zinasema uamuzi huo wa Umoja wa Mataifa unalenga kuisaidia serikali ya Somalia iweze kukabiliana na waasi hasa wanamgambo wa Al Shabaab ambao bado wanaendelea kutekeleza mashambulizi nchini humo.
Imearifiwa kuwa katika kikao chake cha wiki ijayo, Baraza la Usalama litaidhinisha kuongezea muda wa Vikosi vya Kulinda Amani vya Umoja wa Afrika Somalia AMISOM pamoja na kuiondolea Somalia vikwazo vya silaha. Baraza la Usalama liliiwekea Somalia vikwazo vya silaha mwaka 1992 wakati wababe wa kivita walipoanza kuwania madaraka baada ya kuangushwa utawala wa Mohammad Siad Barre. Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia aliyechaguliwa mwaka jana amekuwa akitembelea nchi za Magharibi akitaka vikwazo vya silaha dhidi ya nchi yake viondolewe.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO