Tuesday, March 26, 2013

12 WAUAWA SHAMBULIO LA TALIBAN

Kwa akali watu 12 wameripotiwa kuuawa nchini Afghanistan kufuatia shambulio la wanamgambo wa Taliban mashariki mwa nchi hiyo. Duru za usalama zinaripoti kwamba, wanamgambo wa Taliban wamefanya shambulio katika kituo kimoja cha polisi mashariki mwa nchi hiyo na kupelekea watu 12 kuuawa wakiwemo polisi watano. Taarifa zaidi zinasema kuwa, kituo kimoja cha polisi katika mji wa Jalal-Abad kimeshambuliwa kwa mabomu yasiyopungua saba. Kundi la wanamgambo wa Taliban limetangaza kuhusika na shambulio hilo ambalo limepelekea pia makumi ya watu kujeruhiwa. Nchi ya Afghanistan inaendelea kushuhudia hali ya mchafukoge na ukosefu wa amani, licha ya kuweko vikosi vya kigeni vinavyoongozwa na Marekani ambavyo vinadai viko katika nchi hiyo kwa ajili ya kurejesha amani na utulivu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO