Saturday, March 30, 2013

GHAZA MWENYEJI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA USALAMA WA PALESTINA

Mkutano wa kimataifa wa usalama wa taifa la Palestina umeanza leo katika mji wa Ghaza kwa kuhudhuriwa na shakhsia wa kisiasa na kiusalama wa Kiarabu na wa nchi za kigeni. Mkutano huo umeanza leo na utaendelea hadi kesho Jumapili. Hani al Basusi Mkuu wa Kamati ya Mawasiliano ya Mkutano wa Kimataifa wa Usalama wa Taifa la Palestina ametangaza kuwa mkutano huo utachunguza mipango ya kitaifa ya Palestina, malengo ya Wapalestina na Quds, muqawama, serikali ya ndani ya Palestina na mustakbali wake na pia matukio ya kisasa ya kieneo na athari zake kwa malengo ya Palestina. Hani al Basusi amesema washiriki wa mkutano wa Ghaza watawasilisha mapendekezo na ushauri kuhusu mipango ya taifa ya Palestina na kwamba anataraji kuwa maafisa wa ngazi ya juu wa Palestina pia watachukua hatua katika uwanja huo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO