Saturday, March 30, 2013

UFARANSA KUBAKIZA ASKARI 1000 BAADA YA 2013


Rais Francois Hollande wa Ufaransa amesema kuwa nchi yake itabakiza askari wasiopungua 1,000 nchini Mali baada ya mwaka 2013. Hollande ameongeza kuwa, Ufaransa itaanza kuondoa wanajeshi wake nchini Mali mwishoni mwa mwezi huu wa Aprili na kwamba askari hao watapunguzwa na kufikia 2,000 ifikapo mwezi Julai.
Inafaa kukumbusha hapa kuwa, Januari 11 mwaka huu Ufaransa ilianzisha mashambulizi ya kijeshi nchini Mali kwa kisingizio cha kupambana na waasi kaskazini mwa nchi hiyo, mashambulizi ambayo hayakuidhinishwa na Umoja wa Mataifa. Mashambulizi hayo ya Ufaransa yamesababisha hali mbaya ya kibinadamu nchini Mali na kusababisha maelfu ya watu kuwa wakimbizi ndani na nje ya nchi.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO