Tuesday, March 26, 2013

IRAN YAITAKA UN IZUIE MATUMIZI YA KEMIKALI SYRIA

Dk Ali Akbar Salehi, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameutaka Umoja wa Mataifa kuchukua hatua za kuzuia kukaririwa tena utumiaji wa silaha za kemikali uliofanywa na makudi ya kigaidi nchini Syria. Salehi amemuandikia barua Ban Ki-Moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambapo sanjari na kulaani kitendo cha magaidi wa Syria cha kutumia silaha za kemikali ameutaka umoja huo ufanye uchunguzi kuhusiana na jinai hizo za waasi na kuchukua hatua za lazima za kuzuia kukaririwa tena kitendo kama hicho. Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesisitiza katika barua yake kwa Ban Ki-Moon kwamba, kuna haja kwa Umoja wa Mataifa kutuma timu ya wachunguzi huko Syria ili kufanya uchunguzi kuhusiana na jinai zilizofanywa na waasi hao wanaofanya mauaji kila leo dhidi ya raia katika nchi hiyo ya Kiarabu. Aidha Ali Akbar Salehi amesisitiza kwamba, hatua ya waasi wa Syria ya kutumia silaha za kemikali katika mji wa Halab ni tishio la wazi kabisa dhidi ya amani na usalama na kwamba, hatua hiyo inakiuka wazi sheria za kimataifa na mikataba ya kimataifa hususan mkataba wa silaha za kemikali.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO