Tuesday, March 26, 2013

ISRAEL YAACHIA FEDHA ZA KODI KWA PALESTINA


Israel imesema itaanza tena kuipa mamlaka ya wapalestina fedha zinazotokana na kodi ambazo Israel huzikusanya kwa niaba ya mamlaka ya utawala wa Palestina. Fedha hizo zilisimamishwa baada ya Palestina kuomba na kupata hadhi ya mwanachama wa Umoja wa Mataifa asiye taifa huru.
Tangazo kuhusu kuachiwa kwa fedha hizo ambalo limetolewa na ofisi ya waziri mkuu Benjamin Netanyahu halikutoa maelezo zaidi kwa nini hatua imechukuliwa. Marekani na Israel zilipinga ombi la wapalestina kupandishwa hadhi na Umoja wa Mataifa na kuwa mwanachama asiye taifa.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO