Saturday, March 30, 2013

IRAQ KUPEKUWA NDEGE ZA IRAN ZINAZOELEKEA SYRIA


Iraq imesema leo hii kwamba itaimarisha upekuzi wake wa ndege  za Iran zinazopitia anga yake kuelekea Syria ikiwa ni siku chache baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry kuishutumu hadharani serikali ya Iraq kwa kuzifumbia macho safari za ndege hizo.
Wakati msemaji wa Waziri Mkuu Nuri al-Maliki akizungumzia juu ya kuimarishwa kwa masharti mapya juu ya safari za ndege za Syria zinazoelekea Syria, mkuu wa mamlaka ya anga nchini Iraq amekiri kwamba hakuna ndege zilizopekuliwa tokea mwezi wa Oktoba. Ali Mussawi msemaji wa al-Maliki ameliambia shirika la habari la AFP kwamba kutokana na kuwepo kwa taarifa nyingi zenye kugusia usafirishaji wa silaha wameongeza harakati za kufanya upekuzi. Amesema hakuna mtu aliyawapatia ushahidi bali ni taarifa tu.Alipokuwa katika ziara ya ghafla nchini Iraq Jumapili iliopita Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry aliwaambia waandishi wa habari kwamba alimueleza wazi waziri mkuu kwamba safari za ndege za Iran kupitia anga ya Iraq zinasaidia kuendelea kumuweka madarakani Rais Bashar al Assad na utawala wake nchini Syria.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO