Saturday, March 30, 2013

KOREA YA KASKAZINI YATANGAZA HALI YA VITA NA KUSINI


Korea Kaskazini leo imetangaza kuwa iko katika hali ya vita na Korea Kusini na kuzionya serikali ya Korea Kusini na Marekani kwamba uchokozi wowote ule utakuja kupamba moto na kuwa vita kamili vya nyuklia.
Marekani imesema inalichukulia tangazo hilo kwa makini wakati Korea Kusini kwa kiasi kikubwa imelipuuza kuwa kama ni tishio la zamani lililovalishwa nguo mpya. Huo ni mfululizo wa hivi karibuni kabisa wa matangazo makali kutoka serikali ya Korea Kaskazini ambao umekuwa ukijibiwa na onyo kali kutoka serikali za Korea Kusini na Marekani na hiyo kuzusha wasi wasi wa kimataifa kwamba hali hiyo yumkini ikaripuka na kuja kushindwa kudhibitiwa. Korea Kaskazini imesema katika taarifa kwamba kuanzia sasa uhusiano baina ya Korea hizo mbili utashughulikiwa kwa mujibu wa itifaki ya wakati wa vita.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO