Sunday, March 31, 2013

MISRI KUPAMBANA NA WANAOVUNJIA HESHIMA UISLAM

Wizara ya Wakfu ya Misri ina mpango wa kuanzisha kitengo cha kukabiliana na vitendo vya kuivunjia heshima dini tukufu ya Kiislamu. Sheikh Ahmad Khalil anayehusika na masuala ya miongozo ya Kiislamu katika Wizara ya Wakfu ya Misri amesema kuwa, kuna udharura wa kuanzisha kitengo cha kukabiliana na vitendo vinavyoitovukia adabu dini ya Kiislamu ndani na nje ya Misri. Sheikh Khalil amesema kuwa, kitengo hicho kitafuatilia kila kitendo cha kuuvunjia heshima Uislamu kitakachofanywa ndani au nje ya Misri na kutoa majibu yanayotatikana kwa wale wote watakaoyatovukia adabu matukufu ya dini hiyo tukufu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO