Friday, March 22, 2013

RAIS WA CHINA AZURU RUSSIA

Rais mpya wa China Xi Jinping amewasili leo nchini Urusi kwa ziara yake ya kwanza ya nchi za kigeni tangu kuapishwa kuwa rais mapema mwezi huu. Xi na Rais wa Urusi Vladimir Putin wanatarajiwa kutia saini makubaliano kadhaa hasa ya masuala ya nishati na uwekezaji ukiwemo mkataba utakaopelekea Urusi kuongeza kiwango cha mafuta inachouza kwa China. Xi atazuru mataifa manne yakiwemo Tanzania, Congo Brazzaville na Afrika kusini anakotarajiwa kuhudhuria mkutano wa BRICS unaoleta pamoja mataifa ya Brazil,Urusi,India,China na Afrika kusini.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO