Sunday, March 31, 2013

SAFARI ZA NDEGE ZAANZA TENA KATI YA IRAN NA MISRI


Safari ya kwanza ya ndege ya moja kwa moja kati ya Tehran na Cairo imeanza baada ya miongo mitatu. Ndege ya Shirika la Ndege la Memphis la Misri iliondoka Cairo mapema Jumamosi asubuhi na kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Imam Khomeini mjini Tehran.
Ndege hiyo ilikuwa na abiria kadhaa Wairani wakiwemo wanadiplomasia. Mapema mwezi huu Waziri wa Usafari wa Ndege Misri Wael El-Maadawi alisema safari za ndege kati ya Iran na Misri zitaunganisha miji ya kitalii ya Misri kama vile Luxor, Aswan na Abu Simbel na Jamhuri ya Kiislamu. Iran na Misri zimetilaiana saini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kitalii baina ya pande mbili. Uhusiano wa Iran na Misri ulianza kuboreka baada ya dikteta kibaraka Husni Mubarak kutimuliwa madarakani mwaka 2011 na mahala pake kuchukuliwa na Rais Mohammad Mursi wa harakati ya Ikwanul Muslimin. Rais Mursi alitembelea Iran mwezi Agosti kushiriki katika kikao cha Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote NAM. Rais Ahmadinejad wa Iran naye alitembelea Misri miezi miwili iliyopita kushiriki katika kikao cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO