Sunday, March 31, 2013

WIZARA YA SHERIA YASHAMBULIWA LIBYA

Watu wenye silaha wameishambulia Wizara ya Sheria ya Libya baada ya wizara hiyo kukataa kuwalipa mishahara watu wenye silaha walioshiriki kwenye mapinduzi yaliyomng'oa madarakani Kanali Muammar Gaddafi. Ukurasa wa Intaneti wa al Yaumus Saabi'i umeripoti habari hiyo na kuongeza kuwa, leo watu wenye silaha wameishambulia Wizara ya Sheria ya Libya baada ya waziri wa wizara hiyo kukataa kulipa mishahara ya watu hao.

Mtandao huo umenukuu ripoti mbalimbali zilizotolewa nchini Libya zikimnukuu Waziri Sallah al Mirghani akisema kuwa serikali ya Tripoli italipa mishahara ya vikosi vya polisi na vikosi vilivyoko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani tu. Waziri huyo wa Sheria wa Libya ameongeza kuwa, si tu kwamba makundi ya watu wenye silaha yaliyoshiriki katika mapinduzi nchini Libya hayatalipwa mishahara likini pia serikali itashambulia maeneo yaliko makundi hayo na kuyapokonya silaha kwa nguvu. Taarifa kutoka Libya zinasema kuwa, milio ya risasi imesikika karibu na Wizara ya Sheria ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO