Tuesday, April 02, 2013

VITA VYA DUNIA DHIDI YA UISLAM VYAENDELEA MYANMAR


Imam wa msikiti wa al-Islam wa Washington Marekani amesema kuwa, nchini Myanmar kunaendelea kushuhudiwa vita vya dunia dhidi ya Waislamu huku Umoja wa Mataifa ukiendelea kunyamaza kimya. Sheikh Abdul Alim Mussa amesema katika mahojiano aliyofanyiwa na Kanali ya Televisheni ya Kimataifa ya Press TV kuwa, kuteswa Waislamu wa Myanmar ni sawa na "Vita vya Dunia Dhidi ya Uislamu" na kwamba, Umoja wa Mataifa umeendelea kunyamazia kimya jinai na mauaji dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo. Imamu wa Msikiti wa al-Islam wa Washington Marekani amesema kuwa, Vita vya Dunia dhidi ya Uislamu vinafanyika nchini Myanmar na kwamba, watu wasio na hatia yoyote wanauawa kiholela huku vyombo vya habari vya Kimagharibi vikinyamazia kimya jinai hizo dhidi ya binadamu. Tarehe 20 mwezi uliopita wa Machi, zaidi ya Waislamu 40 waliuawa na misikiti kadhaa kuchomwa moto katika miji kadhaa ya katikati mwa Myanmar. Weledi wa mambo wanaamini kuwa, siasa za kindumilakuwili za Wamagharibi kuhusu haki za binadamu na kulinda utu wa mwanadamu zimechangia katika mauaji ya Waislamu wa Myanmar.
Na Salum Bendera

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO