Sunday, April 28, 2013

CHANGAMKIA NAFASI ZA MASOMO YA BURE NCHINI SAUDI ARABIA


Chuo cha King Abdulaziz kilichopo Jiddah nchini Saudi Arabia kinapokea maombi kutoka kwa wanafunzi kote duniani kwa ajili ya masomo ya kiarabu kwa miaka miwili (2 year Arabic scholarship program). Masomo yanatarajiwa kuanza mwezi wa tisa 2013 inshallah. Program hii inajumuisha huduma muhimu zifuatazo, malazi ni bure, milo mitatu kwa siku na pia chuo kitampatia kila mwanafunzi  pesa ya kujikimu ya mwezi mzima. Moja ya masharti muhimu ili uweze kukubaliwa kusoma katika chuo hicho na kupatiwa huduma kama zilivyoorodheshwa hapo juu, muombaji ni lazima awe ni MWANAUME na awe na umri kati ya miaka 17 hadi 25 TU. Kama huna vigezo hivyo hutapata kudahiliwa. Njia za kupata udahili ni kama zifuatazo:
1. Jaza fomu ya chuo kupitia mtandao kwa link ifuatayo,
2. Tuma barua pepe ya nyaraka zako muhimu kwa ali@kau.edu.sa  kupata taarifa ya nyaraka zinazohitajika, tazama link ifuatayo:
3. Kumbuka mwisho wa maombi ni alhamisi tarehe 15th MAY 2013.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO