Sunday, April 21, 2013

CHUCK HAGEL ZIARANI ISRAEL


Waziri wa Ulinzi wa Marekani Chuck Hagel amewasili nchini Israel hii leo katika ziara yake ya wiki nzima Mashariki ya kati. Katika ziara hiyo Hagel atajadili wasiwasi wa mpango wa nyuklia wa Iran na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria.
Katika ziara yake ya kwanza tangu aliposhika wadhifa huo miezi miwili iliopita waziri huyo pia amepanga kuzungumza na mawaziri wenzake wa eneo hilo juu ya mkataba wa silaha wa euro bilioni 10 utakaozipatia ndege za kijeshi za Marekani pamoja na makombora Israel, Saudi Arabia, na nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu.
Amesema mpango huo wa euro bilioni 10 ni ishara tosha kwa Iran kwamba hatua za kijeshi huenda zikachukuliwa kufuatia mpango wake wa nyuklia. 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO