Sunday, April 21, 2013

LUFTHANSA KUFUTA SAARI ZAKE BAADA YA MGOMO WA WAFANYAZI


Shirikal la ndege la Lufthansa la nchini Ujerumani limesema limefuta nyingi ya safari zake za Ulaya, safari za masafa marefu na hata zile za ndani ya nchi hapo kesho kutokana na mgomo wa wafanyakazi wake wa uwanjani pamoja na wale wa ndani ya ndege.  
Taarifa kutoka kwa shirika hilo imesema imewaweka wafanyakazi 20 kati ya 1,650 kuziba pengo la wafanyakazi waliogoma kushughulikia safari za masafa mafupi hapo kesho Jumatatu na kuonya kuwepo kwa athari kubwa kwa safari za masafa marefu. 
Chama cha wafanyakazi kiliitisha mgomo huo wa kutaka asilimia 5.2 ya nyongeza ya mshahara kwa wafanyakazi wa uwanjani 33, 000 wa shirika hilo la Lufthansa baada ya kushindwa kwa duru tatu za mazungumzo ya malipo ya mshahara na viongozi wa shirika hilo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO