Sunday, April 28, 2013

ISRAEL YAJIBU MAPIGO TOKA GHAZA

Israel imejibu mapigo kwa makombora yaliyovurumishwa kutoka Ukanda wa Gaza kwa kufanya mashambulizi ya kutokea angani katika maeneo yanayotumiwa na wanamgambo wa kundi la itikadi kali za Kiislamu la Hamas, ambalo linadhibiti Ukanda wa Gaza. Jeshi la Israel limesema ndege zake zimelipua kituo kimoja cha kuhifadhi silaha za kundi la kigaidi na kituo cha kufanyia mazoezi cha Hamas. Hatua hiyo inakuja baada ya marokeoti kuvurumishwa kusini mwa Israel siku moja kabla. Pia jeshi hilo limefunga eneo moja muhimu la kuvuka mpaka, wakati maafisa wa afya katika Ukanda wa Gaza wakisema hakuna aliyejeruhiwa katika mashambulizi hayo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO