Saturday, April 20, 2013

ISRAEL YATIWA WASIWASI NA MAJESHI YA MISRI


Hatua ya jeshi la Misri ya kutuma vikosi vyake katika eneo la Sinai imewatia wasiwasi maafisa usalama wa utawala wa Kizayuni. Maafisa hao wamesema wametiwa wasiwasi na hatua ya Misri ya kutuma wanajeshi wake katika jangwa la Sinai bila ya kuwasiliana kwanza na utawala huo. Viongozi wa Israel wameeleza kuwa jeshi la Misri mwezi uliopita lilituma kundi la wanajeshi huko Sharm Sheikh bila ya kwanza kuwasiliana na utawala wa Kizayuni kwa shabaha ya kuulinda mfereji wa Suez na kwamba wanajeshi wengi wa Misri wametumwa katika eneo la magharibi mwa jangwa la Sinai.
Wakati huo huo weledi wa mambo wanasema kuwa kuongezwa idadi ya wanajeshi wa Misri huko Sinai si tu kuwa kumevuruga mlingano wa nguvu za kijeshi, bali hatua hiyo ni ukiukaji mkubwa wa makubaliano ya amani yaliyofikiwa kati ya Misri na Israel.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO