Saturday, April 20, 2013

MSHUKIWA NAMBA 2 WA BOSTON ATIWA NGUVUNI

Polisi nchini Marekani inamshikilia kijana mmoja anayedhaniwa kuhusika na mashambulizi yaliyojitokeza katika mbio za marathon za mjini Boston mapema juma hili. Kijana huyo Dzhokhar Tsarnaev mwenye umri wa miaka 19 alikutwa mafichoni alipokuwa amejihifadhi baada ya mshukiwa mwenzie kuuawa katika majibizano makali ya risasi na polisi umbali wa kilomita kumi kutoka Boston.

Ripoti mbalimbali za vyombo vya habari toka nchini humo zinasema mshukiwa huyo alikutwa amejificha kwenye akiwa na majeraha aliyoyapata katika makabiliano baina yao na polisi ambayo yalipelekea kifo cha kaka yake Tamerlan ambaye ni mshukiwa wa pili katika tukio hilo.

Ndugu hao wawili wanadhaniwa ndio waliotega mabomu mawili karibu na mstari wa mwisho wa mbio za marathon za Boston siku ya jumatatu, tukio ambalo lilisababisha vifo vya watu watatu na wengine zaidi ya 170 kujeruhiwa.

Kamishna wa polisi wa Boston Ed Davis amewaambia waandishi wa habari hali ya mshukiwa huyo ni mbaya sana kutokana na majeraha aliyonayo na anapatiwa matibabu katika hospitali moja mjini humo.

Akizungumza baada ya kukamatwa kwa mshukiwa wa pili, Rais wa Marekani Barack Obama ameapa kuhakikisha wanampata mtu aliyewatumia vijana hao wawili kama chambo ya kutekeleza mashambulizi hayo.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAWAZO YAKO